UVUNAJI ASALI

ASALI YA NYUKI WASIODUNGA (APIS MELIPONINI)

Katika mradi wetu, tunawasaidia wajane kujifunza kuhusu ufugaji wa nyuki –
na pia katika uzalishaji wa asali ya nyuki wanaodunga na asali ya nyuki wasiodunga.

Nyuki wasiodunga (apis meliponini), ambao kuna mamia ya makundi yao madogo hawapatikani katika latitudo ya kaskazani. Wanaishi tu katika maeneo yenye unyevunyevu, joto na katika maeneo ya kitropiki ya dunia.
Kama vile nyuki wakawaida tunaowajua, nyuki wasiodunga wanaishi katika muundo wa tabaka la kijamii na ndiye nyuki pekee ambaye pia huunda kundi la kudumu ambalo hukaa kwenye viota vyake kwa vizazi kadhaa.
Tofauti na nyuki tunaowajua ambao hukusanya asali yao na chavua yake katika masega ya nta yenye pembe sita kwenye mizinga , nyuki hao wadogo huweka asali yao kwenye vyungu vidogo vya mviringo.
Asali ya nyuki wadogo pia ni ya kimiminiko zaidi kuliko asali tunayoijua na ina viambato vingine vinavyofaa hasa kwa uponyaji wa vidonda.
Kwa kuwa saizi ya nyuki wadogo kwa kawaida ni theluthi moja ya ukubwa wa Apis meklifera na koloni zao ni ndogo zaidi, kiasi cha asali kinachopatikana ni sehemu ndogo tu ya kile ambacho nyuki wa asali anawea kukusanya..
Mizinga ya nyuki ya UTOB inatundikwa karibu na makazi ya watu ili kulindwa kutokana na mvua, na ili wadudu wengine ,mchwa, nyanu nk. wasiweze kuingia..
Nyuki wa kawaida wa asali, ( Apis mellifera) anapendelea kutengwa katika msitu wa karibu, katika mizinga maalumu ya mlalo ya Kenya-top-bar.
Aina zote mbili za nyuki zina mimea tofauti ambayo huchavusha zaidi. Nyuki wadogo hupendelea kuchavusha macadamia, mikorosho, na miembe.
Maua ya tikiti maji, matunda ya machungwa na miti ya parachichi hayapepeshwi. Apis mellifera lazima iwachavushe.